
Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema) kimesisitiza
kufanya maandamano kuanzia leo hadi
Ijumaa wiki hii licha ya Polisi kuyapiga
marufuku.
Chama hicho kimesema maandamano
hayo yataenda sambamba na migomo na
mikutano ya hadhara na pia
yatawahusisha wananchi wa kawaida,
taasisi na wafuasi wa vyama
vinavyounda Umoja wa Katiba ya
Wananchi(Ukawa) ambavyo ni CUF,
NCCR-Mageuzi, NLD na DP.
Juzi na jana katika baadhi ya mikoa
wafuasi wa chama hicho walifanya
maandamano...