KARIBU BONGO CORNER ENTERTAINMENT GROUP

Karibu katika site yako iliyo bora na inayokuletea habari mbalimbali zinazoigusa dunia katika nyanja ya burudani zaidi. Kaa mkao wa kuburudika zaidi ndani ya Bongo Corner!!! More

Saturday, February 25, 2012

Mansu-Li ndani ya Club Bilicanas Keshooooo!

JUMAPILI HII 26/02/2012 NDANI YA CLUB BILICANAZ, MANSU-LI & AVELI GHETTO MASSAYA, NA P THE MC WATAFANYA MAMBO SAMBAMBA NA WATEULE - JAYMOE,MOXIE NA JAHFFARAI NA WENGINE KIBAO. KARIBU SANA KWA KIINGILIO CHA SHILINGI 6000/-

Wednesday, February 22, 2012

Sugu na Ruge sasa Amani

Meza kuu ya upatanisho ilikaliwa na Mhe. Emanuel Nchimbi wazili  wa vijana, habari,michezo na utamaduni, Joseph Mbilinyi (sugu) mbunge wa Mbeya mjini, Ruge Mutahaba (Mkurugenzi wa Clouds Media Group) na mbunge wa Singida mashariki Mhe. Tundu Lisu.
Hii ilikuwa katika kutafuta suluhisho la mafarakano yaliokuwepo kati ya Mr. Sugu na Mr. Ruge yaliyofanyika mbele ya waandishi wa habari kwa lengo moja tu la kutafuta huo upatanishi. Sasa Sugu na Ruge wanafungua ukurasa mpya na kufuta yale yaliyopita. Waswahili husema "Yaliyopita si ndwele tugange yajayo"  na sasa tunategemea kuona kauli mpya tofauti na zile zilizopita. Amani kwenu wadau.

Mwanamke wa Wiki

Flaviana Matata mwanamitindo wa kike anayetikisa nje ya bongo na kuifanya Tanzania kung'ara katika tasnia ya mitindo kimataifa. Leo mrembo huyu mwanamitindo ndiye anayetung'arishia ukurasa wetu kwa kuwa ni mwanamke wa wiki ndani ya Bongo Corner. Hii ndiyo aina ya wanawake wanaoitajika katika dunia ya leo yaani kwa maana kwamba, mwanamke anapaswa kujishughulisha na siyo kungojea kuwa mdakaji. Flaviana ni moja kati ya hawa wanawake ninao wazungumzia. Mwanadada huyu kwa sasa anamiliki au anatarajia kumiliki taasisi yake inayofahamika kama Flaviana Matata Foundation. Pongezi za dhati kabisa zinadondoka kwako mwanadada Flaviana toka katika uongozi mzima wa Bongo Corner Entertainment na Mungu akuzidishie katika kazi zako!

Monday, February 13, 2012

Zambia wang'ara

Timu ya taifa ya Zambia imeng'ara katika michuano ya mabingwa Afrika baada ya kuishinda Ivory Coast kwa mikwaju ya penati.
Timu ya Zambia imeiwekea tiafa hilo heshima katika kuwaenzi wachezaji ya zamani wa timu hiyo waliofariki kwa ajali ya ndege mnamo waka 1993.
Kung'ara kwa timu hiyo

Sunday, February 12, 2012

Bobby Brown astushwa na kifo cha Whitney

Mwana muziki Bobby Brown na aliyekuwa mume wa Whitney Houston ajikuta akipagawa ghafla jukwaani kutokana na kupata taarifa za kifo cha aliyekuwa mke wake (Whitney) kilichotokea jumamosi hii.Habari hizi zilimfikia Bobby pindi alipokuwa katika tamasha moja na New Edition huko Landers Center Mississippi.
Bobby alijikuta akikili mbele ya uma mapenzi ya dhati aliokuwa nao juu ya mpenzi wake huyo na kukaliliwa akitamka maneno yaha,"Hawali ya yote napenda kuwaambia kwamba nawapenda sana nyote" Anasema Bobby, "Pili napenda kusema, nakupenda sana Whitney na inaniwia vigumu sana mimi kuwepo hii leo katika jukwaa hili nanyi" mwisho wa kunukuu.
 took the stage with New Edition at Landers Center

Saturday, February 11, 2012

Whitney Afariki dunia!

Whitney Huston enzi za uhai wake
Kwa habari zilizotufikia ni kwamba msanii Whitney Huston amefariki dunia, habari toka CNN zilisema kuwa mkali huyo alikutwa na umauti  mida ya 3:55 p.m katika hotel ijulikanayo kama Beverly Hilton Hotel.
Huston amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 48 tangu kuzaliwa kwake mwaka 1964.
Whitney atakumbukwa kwa kazi nyingi alizozifanya enzi za uhai wake, hususani albamu zake mbili za ukweli  kama "I'm your Baby Tonight," ya miaka ya 90 na "The Bodyguard" kazi iliyotufanyika miaka ya 92.
Salamu za pole ziende kwa wapenzi wote wa mwana mziki huyo hususani kwa yake familia na hasa mwanae wa kike afahamikaye kama Bobbi Kristina. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi Amina!









Rooney aipaisha Man United!

Mabao mawali yaliyofungwa na Wyne Rooney yameipa Manchester United ushindi zidi ya maasimu wao Liverpool katika uwanja wa Old Trafford. Ushindi huo umeifanya timu ya Manchester United kukaa kileleni kwa sasa huku mechi ya maasimu wao wakuu Manchester City ikiwa inasubiriwa kuthibitisha uwepo wao kileleni.
hekaheka kati ya Evra(Manchester United) na Suarez (Liverpool) halikukosekana, ni kutokana na Suarez kukataa kumpa mkono wa kheri Evra kabla ya mech kuanza na Evra kuutupilia mbali mkono wa Suarez alipokuwa akimsalimia goli kipa wa Manchester United (De Gea).
Mpira ulianza kwa kasi kubwa sana huku Manchester United wakioneka na kuumilika mpira kwa hali ya juu lakini mpaka timu zinakwenda mapumziko mabao yalikuwa ni bila kwa bila. Upepo ulikuja kubadilika katika kipindi cha pili dakika ya 47 ambapo Rooney aliipa timu yake bao la kwanza. Mnamo dakika ya 50 Wyne Rooney hakufanya hajizi kwa kuipa tena timu yake bao la pili, lakini ilipofika dakika ya pili Luic Suarez aliipatia Liverpool bao la kwanza ukiwa ni mpira uliochezwa vibaya na beki tegemezi ya Manchester United Ferdinand na Suarez kuusukumia mpira huo wavuni.
Ushindi huo unaipa Manchester Unnited pointi 58 zidi ya 57 ya Manchester City, ikifuatiwa na Tottenham yenye pointi 53 zidi ya Arsenal yenye pointi 43 ikilingana na Chelsea kwa poinnti na wengine wakifuatia.

Thursday, February 9, 2012

Mwanamke wa Wiki

Kutana na Joyce Kiwia katika kurasa yetu ya mwanamke wa wiki ndani ya My Profile. Jua Joyce Kiwia ni nani na kwanini ni Joyce na mengine mengi hapahapa katika site yako ya Bongo corner. Kupitia kurasa hii utaweza kuyafahamu mengi  yanayomuhusu Miss Joyce ambayo yawezekana hauyafahamu au unayafahamu kwa kuyasikia tu.

Wednesday, February 8, 2012

Sasa ni Sungura Sokoni!

Mtambue kwa majina kama Said Salum Sungura a.k.a Sungura hili ni jembe la kale lenye mpini mpya sokoni. Mr Sungura ndani ya 2012 ameamua kuufuta wake ukimya kwa kudondosha Song lake Lifahamikalo kama "Nipangishe" Mr Sungura anaomba zennu hifadhi katika Game hii ya Bongo Flava. Jembe ameongea na BC Crew na kujimwaga mazima kuhusu ujio wake. So kaa tayari kumpokea Sungura!

Mr. Vinapanda bei sasa anasema JIPANGE!

Kaa tayari kwa ujio mpya wa Blad Key (Mr. Vinapanda bei) katika nyimbo yake mpya ijulikanayo kama "Jipange!". Jembe linasisitiza kitu muhimu sote tujipange sasa na siyo tulie au kulalamika kutokana na vitu  kupanda bei.