Sunday, August 21, 2011

Tafakari ya leo

Kama tungekuwa makini tena makini kweli, tusingefika hapa tulipo fika leo kama taifa. Uwezi amini hii Tanzania yenye madini, mito, nchi iliyozungukwa na maziwa makuu, wanyama na ardhi nzuri leo hii ipo kizani. Je mchawi nani? Na nani alaumiwe katika hili mbona wengine mnanufaika na matumbo yenu yananeemeka? Ukisema unaambiwa hauna uzalendo je ni uzalendo gani unaotakiwa hapa. Mmemkana hata mwasisi wa taifa hili

0 comments: