Wednesday, October 22, 2014

MAKAMBA AHAHIDI KUMPIGIA DEBE MWANAE MBIO ZA URAISI 2015

Mbio za urais ndani ya CCM zimechukua sura mpya baada ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusuf Makamba kutangaza rasmi kumuunga mkono mtoto wake, January Makamba.

Akizungumza katika mahojiano maalumu nyumbani kwake Tegeta, Dar es Salaam, Mzee Makamba alisema ameamua kumuunga mkono January kwa sababu anaamini mwanaye ana uwezo.

“Mbali ya kwamba January ni mwanangu, lakini najua ana uwezo, anajua shida za Watanzania kwa kuwa alikuwa msaidizi wa Rais Jakaya Kikwete ambaye walizunguka naye Tanzania na dunia nzima.

“Makamba ni msomi, kijana na Tanzania ya sasa inahitaji rais wa kisasa atakayekwenda na kasi ya dunia na Junuary ni kizazi cha digitali, siyo kizazi cha BBC yaani Born Before Computer ambao hawana uwezo wa kukabiliana na kasi ya dunia ya leo,” alisema.

Mzee Makamba alisema ameamua kufunguka kuhusu msimamo wake huo, baada ya watu wengi kumuuliza anamuunga mkono nani kati ya wagombea waliotangaza nia na ambao bado hawajatangaza.

Alitoa mfano wa mti wa mkomamanga kuwa huzaa komamanga na kwamba yeye atamuunga mkono mtoto wake badala ya mtu mwingine.

0 comments: